Wednesday, 21 August 2013

MADINI YANAYOFAA KWA MAMA MJAMZITO



AINA ZA MADINI YANAYOFAA KWA MAMA MJAMZITO
Aina  ya vitamini  C na madini ya chuma yaweza kupatikana katika maini, maharagwe, mboga zenye majani mabichi, njugu, na nafaka zilizoongezwa vitamini na madini mbalimbali. Kuchanganya chakula chenye vitamini ya C, kama matunda yaliyotoka shambani karibuni, pamoja na chakula chenye madini ya chuma huongeza madini hayo mwilini.
Ongezeko linalopendekezwa kwa mwanamke mwenye uzito unaofaa anapokuwa na mimba ni kilogramu 9 hadi 12 kufikia wakati wa kujifungua. Hata hivyo, wasichana au wanawake ambao hawakuwa wakila chakula cha kutosha wanapaswa kuongeza kati ya kilogramu 12 hadi 15, na wale wanene wanapaswa kuongeza kilogramu 7 hadi 9 tu.

MADOKEZO YA KUWASAIDIA WANAWAKE WAJAWAZITO
● Kila siku mwanamke mjamzito anahitaji kula matunda, mboga (hasa zilizo na majani ya rangi nzito ya kijani, na zenye rangi ya machungwa, au nyekundu), maharagwe mbalimbali (kutia ndani soya, dengu, na njegere), nafaka (kutia ndani ngano, mahindi na shayiri - hasa zile ambazo hazijatolewa maganda au zilizotiwa vitu vingine), chakula kinachotokana na wanyama (samaki, nyama ya kuku, nyama ya ng’ombe, mayai, jibini, na maziwa, hasa yale ambayo yametolewa mafuta). Mafuta, sukari na chumvi vinapaswa kutumiwa kwa kiasi. Kunywa maji mengi. Epuka vinywaji vyenye kafeini, na vyakula vilivyotiwa dawa za kuhifadhi na kemikali nyinginezo (kama za kutia rangi na ladha). Wanga, udongo wa mfinyanzi, na vitu vingine visivyoliwa vyaweza kusababisha utapiamlo na kumtia sumu.

● Jihadhari na hatari ya mambo yanayochafua mazingira, kama minunururisho ya eksirei na kemikali hatari. Punguza utumizi wa dawa za kupulizia na dawa nyingine za nyumbani. Usijipashe joto kupita kiasi kwa kukaa mahali penye joto sana au kwa kufanya mazoezi sana. Epuka kusimama kwa muda mrefu na kujikaza kupita kiasi. Funga mkanda wa usalama vizuri.

No comments:

Post a Comment