Tuesday, 31 May 2016

MWANAMKE NA FAMILIA: JE UPO TAYARI

MWANAMKE NA FAMILIA: JE UPO TAYARI: Habari, Napenda kutumia nafasi hii kuzungumza na kijana mwenzangu ambaye anasoma/ kujifunza kupitia makala hii, kuna mambo mawili au matat...

JE UPO TAYARI

Habari,

Napenda kutumia nafasi hii kuzungumza na kijana mwenzangu ambaye anasoma/ kujifunza kupitia makala hii, kuna mambo mawili au matatu ambayo ningetamani tushirikishane siku hii ya leo, ambayo naamini kwa namna moja ama nyingine yanaweza kubadili mtazamo wako juu ya haya tutakayojadili.

                                                MAHUSIANO YA KIMAPENZI

Mpendwa wangu, napenda nifahamu unalichukuliaje neno hili 'Mahusiano ya kimapenzi' Je? lina uzito wowote au ni neno la kawaida? Na kama lina maana yoyote kwako naomba usisite kunitumia ujumbe wa email katika email hii dianashirima47@gmail.com ili nifahamu jibu lako, na kama kuna swali lolote la binafsi usisite niulize mitakujibu.


1. Katika safari yako yako ya ujana ni changamoto zipi umekutana nazo katika swala zima la mahusiano ya kimapenzi

2. Ulipoanza safari hii ni nini kilisababisha uingie katika safari hii

3.  Ni faida gani umeipata/ hasara zipi umepata baada ya kuingia katika safari hii

4. Ushauri wako ni nini kwa vijana walio nyuma yako ambao hawajaingia katika safari hii ya mahusiano ya kimapenzi.



  • Hayo ni baadhi ya maswali ambayo nimekuwa nikiwauliza baadhi ya vijana niliobahatika kukutana nao na kuongea nao, natamani kupata majibu yako pia wewe unaesoma makala hii.
Karibu sana tujifunze pamoja, nitaendelea na makala hii mara tu nitakapopokea email zenu na kuzisoma kisha nitarudi na majibu na somo letu lililobakia.




Imeandaliwa 
Diana D. Shirima - Mwanaharakati.  dianashirima47@gmail.com



Wednesday, 6 November 2013

SABABU ZINAZOZUIA KUOA/ KUOLEWA



SABABU INAYOWAFANYA WANAWAKE NA WANAUME WENGI KUTOTAKA
KUOA/ KUOLEWA.
Katika maisha ya vijana wengi wa sasa, tumekuwa kukishuhudia vitendo vingi vya ukatili kwa wanandoa kiasi ambacho tumepoteza imani sana katika kufikia maamuzi ya kuoa/ kuolewa.
Kwa muhtasari tuu, ningependa tuchambue sababu mbali mbali ambazo kiukweli zimekuwa kiongozi katika kuhakikisha thamani ya kuoa/ kuolewa inashuka au kupotea kabisa. Na kwa kila kijana ambaye anapenda kubadilika na kujifunza atapata kitu kipya katika makala hii na hivyo kufunguka kwa namna moja au nyingine katika swala hili gumu ambalo ndani ya miaka michache ijayo litakuwa janga la kitaifa.

Baadhi ya sababu hizo ni kama ifuatavyo;
-         Kuingia katika mahusiano ya kimapenzi kabla ya wakati, hii tukimaanisha katika umri mdogo.
-         Kushuhudia ukatili wa wazi wazi katika familia uliyoishi au jamii inayokuzunguka ndani na nje ya familia yako.
-         Kupata habari za kukatisha tamaa kutoka kwa wakubwa zako ambao kwa namna moja ama nyingine wamekuwa wakikushuhudia kushuka kwa thamani ya kuoa/ kuolewa.
-         Mfumo mbovu wa maisha unayoishi kijana, kwa kuamini kuwa vigezo na tabia unazohitaji kwa mke/ mume unayemtaka havijaonekana/ kukupendeza, hivyo unajikuta ukichagua sana.
-         Mara nyingine ni maudhi na kuumizwa nafsi kutoka kwa mpenzi aliekuacha/kumuacha bila sababu za msingi n.k
Kiukweli vijana wengi tuna mitazamo mbali mbali kulingana na uchaguzi sahihi juu ya nani anastahili/kufaa kuwa mwenzi wa maisha yangu, lakini tunakosea sana hasa inapokuja katika maamuzi,.

Nimeshuhudia vijana wengi wakipoteza muda katika kuchagua na kuandika vigezo vyao ambavyo wanahisi ndio key point ya kupata mwenzi, bila kusahau/ kuangalia upande mwingine wa shilingi, kwamba ‘ Mimi ninavigezo gani kulingana na hivi?’
Jiulize swali hili kijana unayesoma makala hii, wewe ni PERFECT? 

Na unahisi umekamilika sana kuwa na huyo unaemtaka? Mungu hawezi kukupa mwanamume/ mwanamke perfect kama wewe mwenyewe njia zako hazijatimilika.
Hivyo cha msingi hapa ni wewe kujitambua, kuangalia njia zako zipoje na sasa uingie katika swala la imani na kumuomba Mungu akupe mtu sahihi, ama sivyo utakuwa ukiwaona wanaume/wanawake wote ni wabaya/si waaminifu katika ndoa, na kubaki mpweke kwa maisha yako yote.
Jifunze kusamehe na kusahau, kisha fanya mambo yako kwa mpangilio utaona faaida zake.
Usife moyo tuzidi kuwa pamoja na tutafundishana na kusaidiana kila wakati,


Imeandaliwa na Diana D. Shirima
Founder - Wanawake Mashujaa Tanzania

ELIMU JUU YA KUOA NA KUOLEWA



KUOA AU KUOLEWA
Maamuzi ya kuoa au kuolewa, si maamuzi madogo, ni moja ya maamuzi makubwa ambayo vijana wengi wa kike na wa kiume wana kutana nayo kila siku. Sasa katika kufanya maamuzi haya ukweli ni kwamba sehemu kubwa ya vijana mpaka wafike mahali pa kumpata kijana au binti wa kusema huyu ndiye haswa wa kuoana nae , basi ujue tayari wengi wanakuwa walishakosea mara nyingi mpaka kufikia hapo. Wapo ambao wakikosea husema, yule wa kwanza hakuwa chaguo langu, au haukua mpango wa Mungu mwenyewe bali malaika, au utasikia mwingine akisema Mimi sina uhakika sana na wewe kuwa mwenzi wa kudumu.

Je hivi kweli hayo ndiyo yalivyo au ni ujanja ujanja tu wa vijana tena hasa wa kiume ndio wenye kauli kama hizi. Lengo la makala hii kwako kijana mwenzangu ni kutaka kukueleza sababu kadhaa ambazo hupelekea vijana wengi kufanya makosa katika kutafuta mwenzi wa maisha.

vijana Wengi wanakuwa tayari wameshafanya maamuzi yao wenyewe.
Vijana wengi huwa wanaomba Mungu awape mtu sahihi wa kuishi naye katika maisha yao na wakati huo huo tayari kwenye nafsi yake anakuwa na mtu ambaye ndiye chaguo lake wakuishi Naye kwa sababu hiyo ina kuwa ni vigumu kwao kumpata mtu wa mapenzi ya Mungu na pia ina muwia kazi Mungu kukuonyesha mke au mme wa kusudi lake kwani tayari umeshafanya maamuzi ndani yake, je Mungu afanye nini kama sio kunyamaza.

Sababu zinginezo
Hapa nitaelezea mambo mawili kwa wakati mmoja, la kwanza ni hili kuna vijana huenda wao wenyewe au ndugu zake, wazazi wake walishawahi kumtoa huyo mtoto kama sadaka kwa mapepo kwa sababu ya mila zao au pia alipatikana kwa njia za kipepo. Siri moja ni hii kuna baadhi ya mapepo huwa hayapendi kushare sex na mtu mwingine, hivyo ni lazima yalete kila namna ya upinzani ili mtu asiolewe na wala kuoa. Na mwingine hata kama hakutolewa kama sadaka lakini huenda pepo wameshawahi kufanya mapenzi na huyo mtu na kama yatampenda basi ujue hayatakubali aolewe au kuoa, hivyo yatamletea kila namna ya upinzani katika kuolewa au kuoa kwake. Mengine hufika mahali hata pa kumwachia kijana wa watu harufu mbaya ili mwingine asimpende.

Maneno ya kujitamkia mwenyewe
Kuna baadhi na hasa hapa ni akina dada kwa sababu mbalimbali kama vile kubakwa, kujeruhiwa katika nafsi kwa sababu ya kuachwa na mchumba wake hufikia mahali wakasema mimi sitaki tena kuolewa. Sasa inapofika muda umepita na wanataka tena kuolewa wananaza kuomba Mungu awape mume, wakati huo wamesahau kwamba walishatamka kwamba hawataki tena kuolewa. Nisikilize ukisema hutaki kuolewa au kuoa tena, maana yake unaifunga nafsi yako hapo kwamba hutaoa au kuolewa, na Biblia inasema mtu atashiba matunda ya kinywa chake. Na wakati huo shetani ni mwepesi kufuatilia maneno ambayo ni ya athari kwako. Sasa bila kuondoa hayo maneno kwanza katika nafsi yako na kisha kumuomba Mungu akusaidie katika uamuzi sahihi itakupa mud asana kufikia lengo la kuoa au kuolewa.

Dhambi/ Maswala ya kiimani
Sikiliza Biblia inasema afichaye dhambi zake hatafanikiwa, (Mithali 28:13a). Kuna baadhi ya vijana huwa wanakuwa awali kuna baadhi ya dhambi wamezifanya na hawajazitubia, na bado wana taka mtu awaoe au wa kumwoa. Biblia iko very clear kama kuna dhambi umeficha hutafanikiwa, sasa inategemeana, lakini pia inahusiana sana na kutofanikiwa kwako pia kumpata hata mwenzi tu. Nikupe mfano mara nyingi watu wanatoa mimba, au watoto wanaozaa, nao pia kupata mume au mke huwa inakuwa kazi kweli kweli.

Kutokuenenda kwa Roho.
Paulo anasema, “Basi nasema enendeni kwa roho wala hamtatimiza kamwe tama za mwili” (Wagalatia 5: 16). Kuenenda wa Roho maana yake ni kuongozwa na Roho Mtakatifu, hii ni pamoja na zoezi zima la kutafuta mke au mume. Sasa kwa sababu wewe unaenda kwa mwili, mara eti nataka mtoto portable, mguu wa chupa, mweupeee, nk. Hivyo vitu unavyotaka wewe kuna wengine pia wanataka hivyohivyo na matokeo yake mnaanza kugombaniana msichana au mvulana kwa sababu tamaa za miili yetu zinawaongoza huko.

Kuwa na vigezo binafsi.
Vijana wengi sana katika suala zima la kupata mke ua mume, ukweli wengi wao wana vigezo vingi sana ambavyo kila mmoja angependa huyo mchumba wake awe navyo. Utasikia lazima awe wa kabila ya kwangu, awe portable, mweupee, mrefu ndio mzuri, ajue kutabasamu na kisha awe ana ulamba. Sawa mi sikatai hivyo vigezo, lakini nikuulize swali Je! Unayajua mawazo ya Mungu kuhusu wewe kwa habari ya mkeo au mumeo? Je kibiblia na kijamii hivyo vigezo vyako vinakubalika/ na je mke/mume mtu huchagua mwenyewe au hupewa na Bwana,  Najua utaniambia mimi nitaomba Mungu anipe mke/mume mwenye sifa hizo. Ok. Ukiniambia hivyo na mimi nitakuambia kumuomba Mungu kwa muundo huo ni nzuri kabisa, wala sio dhambi lakini kumbuka maandalio ya moyo ni ya mwanadamu lakini jawabu la ulimi hutoka kwa Bwana. Na hapo ndipo patamu, wengi huwa wanaomba kwa vigezo vyao, na mara nyingi Mungu anapojibu inakuwa tofauti na vigezo vyao, na hapo wengine wanakataa hata chaguo la Bwana wanabakia kuteseka. Jua kwamba wewe unapoweka vigezo vya mwenzi wako na Mungu naye ana vigezo vya aina ya mwenzi anayekufaa.

Kufanya maamuzi kabla ya wakati.
Biblia inasema katika Mhubiri 3:1 “kwa kila jambo kuna majira yake, na wakati wa kila kusudi chini ya mbingu”.Hili ni jambo la kawaida, hata wakati wa uchaguzi kura mtu harusiwi kupiga kama hajafikisha miaka kumi na nane kwa nchi nyingi. Vivyo hivyo hata suala la kutafuta mke au mume lina wakati wake maalumu. Ukitaka kulifanya nje ya kipindi ambacho Mungu amekipanga kwa ajili yako utateseka hadi uchoke. Kumbuka kila mtu ana muda wake, hivyo basi hakuna muda maalumu wa kila mtu kuanza kutafuta mke au mume, bali kila mtu ana muda wake na mara tu unapowadia Mungu humjulisha mtu wake.
Nisikilize ukiulekeza moyo wako upate kujua haya nisemayo na ukajizuia kufanya makosa kama haya, basi nataka nikuhakikishe suala la kupata mke au mume wa kutoka kwa Mungu litakuwa ni jepesi sana,ni sawa sawa na kuombea chakula na ukishafumbua macho ukaanza kula moja kwa moja ukiwa na uhakika kimeponywa na kubarikiwa. Kwa ushahuri zaidi endelea kufuatilia makala hizi na kupenda kujifunza zaidi, bila kuacha kumuomba Mungu.

Imeandaliwa na;
DIANA D. SHIRIMA
Founder - Wanawake Mashujaa Tanzania
 

UKAMILIFU WA MWANAMKE KATIKA FAMILIA/MAISHA YA NDOA


UKAMILIFU WA MWANAMKE KATIKA FAMILIA/MAISHA YA NDOA

Ukamilifu wa mwanamke sio tu kujua aina za mapishi, kutoa penzi, kuwa mwepesi wakati wa kungonoana, mwenye kulipenda umbile lake zuri alilojaaliwa na Mungu, usafi na mwenye kuvutia bali pia uwezo wa kujua kumuwahisha mpenzi hasa kama mpenzi wako ni mmoja kati ya wale waliojaaliwa kwenda "mwendo mrefu" au kazoea kujizuia na hivyo anashindwa kujiachia ili awahi kufika kileleni.
Au inawezekana kabisa bao la kwanza kutoka kwa mpenzi wako linakuja haraka (kawaida kwa wanaume wengi hasa kama anahamu sana) lakini yatakayofuatia yanachukua "mwaka" hali inayoweza kukufanya usitake kumuona mpenzi wako anakuja tena na tena....

Unaweza kujitahidi kumfanyia manjonjo na masham-sham ili anashindwa kujizuia na kumaliza mapema lakini njemba haifiki walanini.....hii ikitokea usikate tamaa na kujishtukia kuwa huwezi "game"...."game" unaiweza ila hujampatia tu......sasa nitakupa mbinu ambayo mwanaume yeyote hawezi kujizuia ikiwa utazipatia mbinu  hizi.
Kumbuka unapofanya hii mbinu lengo ni wewe na yeye kufurahia hivyo haijalishi ikiwa mtafika wote au yeye kuanza.........utahisi mchanganyiko wa hisia za raha, furaha, ukamili kama mwanamke na mapenzi ya dhati kwa mpenzi wako......inategemea zaidi na unavyolichukulia tendo hili takatifu, kama ni mpenzi wa tendo hili kama mimi basi utakuwa umenielewa vema.

Mkao-Kama kawaida mkao ni kifo cha mende
na mtindo ni mwanamke chini.....kifo cha mende ni mkao wenye mitindo mingi ambayo haichoshi na inakuwezesha wewe mwanamke kuwa in control na kuwa huru kumfanyia mume/mpenzi wako mambo mengi kwa kutumia uke wako kuliko mikao migine.

Si kwa vile nimesema kifo cha mende basi wewe unakimbilia kitandani na kujilaza chali na kujipanua.....hapana! Cheza-cheza nae mpe ile inaitwa "stata", au "hapitaiza" kabla ya mlo kamili (hajalishi ni mzunguuko wa ngapi)....si unajua kuwa kila bao lina utamu tofauti??

Ili asijue nia yako ni nini basi unapaswa "kuzuga" na kumlaza yeye pale kitandani na kuanza kumfanyia "uchunguzi wa kina" kwa kutumia mikono/vidole, matiti, midomo, ulimi, mashavu ya uke.....na hakikisha unagusa kila kona ya mwili wake ambayo wewe unajua anapenda kuguswa.
Jitahidi sana kuwa na utaratibu ili usiharibu mambo, maana mwanaume mwenye utaratibu atakushangaa sana pale unapofanya makeke mengii bila mpangilio.

Mazingira ya chumbani, jikoni na chumba cha watoto.
Mwanamke anapaswa kuhakikisha kila siku anapo amka kitanda chake kiwe safi kwa kuangalia mazingira ya chumba kizima ikiwemo mashuka, vitaulo vidogo n.k, ukimaliza angalia choo chenu kama ni kisafi na kama unaona kuna usafi basi safisha maraa moja, kasha angalia jikoni ambapo ndio afya ya familia nzima inategemea, safisha jiko na kuweka mazingira ya jiko katika hali ya usafi kabisa.
Sehemu nyingine ni chumbani kwa watoto, endapo una vyumba tofauti kwa ajili ya watoto unapaswa kuvikagua na kuhakikisha vinabadilishwa mashuka na kufanyiwa usafi kila siku. Wafundishe pia watoto kufanya usafi wenyewe katika vyumba vyao hii itasaidia kuwaandaa watoto katika msingi mzuri wa maisha yao.
Hapa nimejaribu kuchambua zaidi kwa undani kila sehemu ya nyumba;
Jikoni...
Chumba hiki kinahitaji kua na mwanga wa kutosha kulingana na ukubwa wa jiko. Unaweza kuweka taa zaidi ya moja kwani husaidia jiko kua safi, usalama etc. Naomba ijulikane kua chumba hiki kina vitu vya hatari kama jiko, fridge etc... Sasa basi ukiweka taa za kwenye dari, za ukutani zitakusaidia sana kutoa mwanga unaohitajika na uta akisi rangi ya ukutani na vyombo vyako ambapo utapata muonekano mzuri.

Chumba cha kusomea/home office:
Chumba hiki mwanga ni muhimu, kumbuka ni sehemu ya kusomea na kuandika etc. Sasa mwanga hafifu utaweza kuharibu macho yako. Kama chumba chako hiki ni kikubwa na deski limewekwa katikati ya chumba, basi socket ya umeme inahitajika kuwekwa level ya sakafu, kwa juu kidogo ili kusaidia kutokua na nyaya nyingi na zinakua na mpangilio.
Mwangaza katikati ya desk husaidia kufanya chumba kidogo kuonekana kikubwa.

Bafuni..
Hapa kunahitaji mwanga zaidi ambao utakuwezesha kuona vizuri, lakini pia mwangaza huo unahitaji kua sawa yaani ukitaka unaweza  kupunguza ama kuongeza, maana siku hizi tunajenga mabafu mazuri ya kisasa, ambayo unaweza kupumzika pia. Hii ni kwa  mara chache inatokana na kuhusishwa na mwanga ama sakafu ambazo zimewekwa kwa usadi na kwa mpangilio mzuri na huonyesha umaridadi wake.

Chumba cha kuchezea watoto:
Chumba hiki kinahitaji usalama zaidi, taa ziwe ni za juu ama ukutani, kusiwe na mrundikano wa vitu, weka taa ambazo mwanga wake unaweza kuupunguza, kuto kuweka vitu sakafuni ambavyo ni hatarishi. bila kusahau mapazia, pia yanatakiwa kua yanafungwa vizuri, kuzuia watoto kuchezea maana yanaweza kudondokea watoto.


Chumba cha kulia chakula:
Chumba hiki kinahitajika kua na mwangaza wa wastani. Taa za ukutani, taa za picha(urembo) za ukutani na taa za mezani ni chaguo lako.  Unaweza ukapata mwanga wa kutosha kuzunguka meza kwa kutumia taa za glopu ndoga ama taa ya kuning'inia ama zote kwa pamoja
Taa zenye mwanga mdogo huongeza nakshi ya muonekano sehemu ya kulia chakula..

Chumba cha kulala:
Chumba huhitaji mwanga mdogo muda mwingi, japo kua mpangilio mzuri wa taa unahitajika ili kupata mwanga unaohitajika kwa ajili ya usafi na kufanya shughuli zingine kama kukunja nguo, kupaki vitu, kuvaa etc. Hii inaweza kutolewa/kuwezeshwa kwa kuchanganywa kwa taa za ukutani, taa za juu ambazo zinaweza kua na mwanga hafifu (zinazopunguzika na kuongezeka mwanga) hua na muonekano wa kuvutia.


Mwanga mzuri wa taa za pembeni ya vitanda (bedside lamp/lights) ni mfano mzuri. Hii inamaanisha, weka taa ambazo ni maalum kwa kusomea(reading lights/bedside lamps). waweza weka taa zenye urembo, rahisi kutumia, na zinazodumu na zenye kuvutia.

NB: Naomba ieleweke kua kabla ya kununua taa jitahidi sana ujue ina mwaga wa kiasi gani, na kama ina matumizi gani,... maana unaweza nunua taa ilimradi taa tuuu, kumbuka kuna vyumba havi hitaji mwanga sana, na kuna vingine vinahitaji mwanga, sehemu kama jikoni, mwanga ni lazima wa kutosha, kwenye vyumba vya watoto kuchezea, nje etc.... ila kwa mahali kama chumbani mwanga mwingi hauhitajiki... maana hapa ni sehemu ya kupumzikia so hakuhitaji sana mwanga, na ninashauri chukua taa ambazo zinapunguzika mwanga kama nilivyoongea hapo juu. hebu fikiria umerudi umechoka kazini,halafu unaingia chumbani unawasha taa, mwanga huooooo, si utaumwa na kichwa wewe jamani?  ............

Usafi Unamaanisha Nini Hasa?
Usafi maana yake ni kitu au mahali kuwa katika hali ya mpangilio na kuruhusu hewa safi iweze kupita, wengi wamekuwa wakipuuza swala la usafi kutokana na uchovu au uvivu, sasa tuchambue tena jambo hili hasa katika suala zima la kitandani na mambo ya faragha.
USAFI WA CHUMBA
Linaweza lisionekane kama ni jambo kubwa na muhimu, lakini nataka kuwahakikishia kwamba, usafi wa chumba ni kati ya vitu muhimu sana vya kuzingatia kabla ya kuingia faragha na mwandani wako.

Hili ni jukumu la wanawake zaidi, lazima uhakikishe chumba kinakuwa kisafi, kuanzia mashuka na vitu vingine vilivyomo chumbani. Mpangilio mzuri wa chumba na usafi kwa ujumla vinamsogeza mwenzi wako karibu zaidi na tukio husika.

Chumba kinapokuwa kichafu, kina harufu mbaya kinapoteza ladha ya kile kinachotarajiwa kufanywa, hali ambayo inaweza kusababisha mafanikio ya kazi yenyewe kuwa madogo sana.

PUPA
Kuna baadhi ya wanaume wana tabia ya kuwa na pupa uwanjani. Hii ni kero kubwa sana. Faragha inahitaji maandalizi, sasa unapoingia uwanjani bila ‘kupasha’ kwanza kwa mazoezi madogo madogo ni wazi timu lazima ifungwe!

 KUZUNGUMZIA MAKOSA
Unapoingia uwanjani halafu utake kifanyike kikao cha usuluhishi juu ya mambo aliyokufanyia mpenzi wako, ni kosa. Kufanya hivyo, kunapunguza utayari kwa kazi mnayotarajia kuifanya.

KUTAWALA
Kwa bahati mbaya sana, wanaume ndiyo wamekuwa na tatizo hili zaidi. Wanakuwa watalawa mchezoni, hawataki maelekezo, wanafanya vile wanavyoona inafaa. Baadhi yao hawataki wenzi wao waoneshe makeke, jitahidi kumkaba kimahaba mwanzoni mwa game ili awe anakusikiliza wewe katika uwanja wa mechi.

Wengine huenda mbali zaidi, huwapiga marufuku wenzi wao wasijishughulishe kwa chochote na inapotokea wakifanya hivyo, huwajia juu wakidai kwamba ni wasaliti ndiyo maana wakawa wataalamu sana. 

 UKALI
Rafiki zangu mapenzi ni burudani, sasa unapopeleka ukali katika eneo hilo unapoteza maana kabisa. Kuwa na lugha tamu, acha maneno makali. Ikitokea kuna mahali panahitaji maelekezo basi yatoe kwa sauti ya mahaba zaidi na siyo kelele, lawama na sauti ya juu.
Ukifanya hivyo unampotezea mwenzako msisiko na mwisho utakayokuwa umefanya yanakuwa kazi bure

 KUDHARAU HISIA ZA MWENZIO
Suala la kusikiliza hisia za mwenzako si ombi, ni kanuni za mapenzi! Utakuta mwingine anakazana kumfanyia kitu fulani mpenzi wake, akiamini anamfurahisha, kumbe ni kinyume chake.
Ikiwa mpenzi wako amekueleza wazi kuwa unachokifanya hakimfurahishi, heshimu hisia zake na ufanye anachokipenda ili mkitoka uwanjani wote muwe mmeridhika.

 MANUKATO MAKALI
Kuna rafiki zangu baada ya kuoga usiku kabla ya kulala, hujipulizia manukato, jambo hili si sahihi. Unapokuwa faragha na mwenzi wako, epuka kujipulizia manukato hasa makali.
Inapendeza zaidi kama mkikutana katika eneo hilo, mkiwa na harufu zenu ‘natural’ zaidi kuliko kero ya manukato. Tatizo hili lipo kwa wanawake zaidi.

 KUMUACHA NJIANI
Hili ni tatizo kubwa na muhimu kuliko yote, hakuna aibu kama hii rafiki zangu. Kwa bahati mbaya, wengi huwa hawasemi, lakini madhara yake ni makubwa.
Si rahisi kueleza kila kitu hapa, lakini elewa kwamba kuanza safari pamoja na mwenzako, halafu njiani unamkimbia na kumuacha porini, ni tatizo kubwa sana katika uhusiano.

Katika shule tunafundishwa kuwa safi saa zote. Tunahimizwa kuoga kila asubuhi kabla ya kuja hapa; pia tunaambiwa kupiga mswaki na kuvaa nguo safi. Kila mwanafunzi anatakikana awe na kucha fupi. zisizokuwo na uchafu ndani yake Kwani uchafu kama huo unaweza kuingia tumboni wakati tunapokula chakula bila kutumia vijiko. Hii pia ndiyo sababu tunaambiwa tutumie vijiko wakati wa kula chakula. Wanafunzi wote ni lazima wachane nywele zao, na pia kuzikata kila mara zinapokuwa ndefu sana. Mtoto mwenye nywele ndefu huwa anatisha, wala havutii.
Hata mahali tunapoishi pia panatakikana pawe safi. Hii ndiyo sababu kila mara asubuhi huwa tunafagia na kuchoma takataka ambazo mara nyingi huwa zinavutia mainzi ambao nao huleta maradhi ya kuumwa na tumbo. Madarasa pia hufagiliwa na kunyunyiziwa maji ili yasiwe na vumbi kwani vijidudu vya magonjwa hujificha katika vumbi kama hilo.
Jambo hili la usafi si la shuleni tu, la! Hata huko nyumbani ni lazima tuone kwamba kila kitu ni safi kama vile sahani tunazotumia kwa chakula, vijiko, meza. na kadhalika. Sufuria zinazopikiwa chakula ni lazima zioshwe kabla ya kuzitumia. Kisha zioshwe tena baada tu ya kuzitumia kwani zisipooshwa mara moja mainzi huzichafua. Kukiwa kuna chakula mezani ni lazima kifunikwe ili kisiguswe na wadudu wenye uchafu.
Wakati wa kulala, yapasa tujifunike nguo na hata ikiwezekana, tutumie chandarua ili tusiumwe na mbu ambao hueneza homa. Pia walimu hutuambia tufungue madirisha wakati wa kulala ili tuvute hewa iliyo safi kila wakati kwa sababu mtu akilala katika chumba ambacho hakina hewa safi huvuta ile hewa chafu ambayo ameitoa yeye mwenyewe naye akiamka hujiona amechoka kama ambaye alikesha akifanya kazi na hali ametoka kulala tu.
Maswali
1.         Ni mambo gani ambayo twaambiwa tuyafanye kabla ya kuja shuleni?
2.         Kucha zikiwa ndefu hujaa nini?
3.         Kwa nini tunaambiwa tutumie vijiko wwakati wa kula?
4.         Nywele za mwanafunzi zinatakikana ziwe fupi au ndefu? Kwa nini?
5.         Kwa nini ni lazima kufunika chakula kikiwa mezani?
6.         Vijidudu vidogo vya maradhi mara nyingi hujificha wapi?
7.         Mtu aliyelala katika chumba ambacho hakina hewa safi, hujisikiaje wakati akiamka asubuhi?
8.         Mainzi huenza ugonjwa gani hasa?
9.         Kwa nini ni vizuri kutumia vijiko wakati wa kula?
10.       Je, wewe unfua nguo zako mara ngapi kwa wiki moja?
Masomo ya Msingi, kitabu cha 4, kur. 79-80 [Maandishi asilia yamegeuzwa kidogo]

USAFI WA MWILI WA WATOTO NA UMUHIMU WAKE


Makala hii inahusu usafi wa mwili na umuhimu wake kwa watoto. Natumai kuwa mtanufaika nayo.
Wazazi na walezi wanaweza kuwa na nafasi kuu na muhimu katika makuzi na usafi wa mtoto, masuala ambayo atakuwa nayo katika maisha yake ya kila siku. Kitendo cha kumfunza mtoto kuhusu usafi wa mwili ni njia bora kabisa ya kumuepusha na maambukizo na maradhi mbalimbali. Ni jukumu la mzazi au mlezi kumfunza mtoto misingi sahihi ya usafi wa mwili wakati mtoto akiwa na umri mdogo kabisa, jambo ambalo litamsaidia mtoto huyo na familia yake katika maisha yao ya baadaye. Misingi ya usafi inapaswa kufundishwa na kuwa sehemu moja ya maisha ya kila siku ya mtu, na pia kuwa njia bora ya wazazi kuwafunza watoto wao kuhusu usafi wa miili yao, kwanza kabisa kwa wazazi hao kuwa mfano mbele ya watoto. Maambukizo ya magonjwa hupungua miongoni mwa watoto wakiwa mashuleani, kwenye maeneo wanayochezea na kadhalika, iwapo watakuwa wamefunzwa namna ya kujilinda na maradhi kwa kuweka miili yao safi na kwa kufuata kikamilifu kanuni za afya kila siku. Mambo ya kuzingatia katika usafi wa mwili wa mtoto yako mengi, lakini hapa nitaorodhesha kwa kifupi haya yafuatayo: Usafi wa Kinywa. Meno na kinywa vyote vinapaswa kuwa visafi wakati wote ili kuzuia magonjwa ya meno na fizi. Aidha usafi wa meno kwa mtoto ni muhimu ili kuzuia kuoza na kuvunjika kwa meno akiwa na umri mdogo. Upigaji mswaki wa mara ka mara, yaani kabla ya kifungua kinywa na baada ya chakula na kabla ya kulala usiku unashauriwa kwa watoto. Upigaji mswaki baada ya kula vyakula vyenye sukari pia ni muhimu kwa watoto, ili kuzuia meno kuoza na harufu mbaya. Pili, uoshaji mikono ni jambo linalopasa kuzingatiwa sana kwa watoto, baada ya kutoka msalani, kabla ya kula au kushika takataka au vitu vingine vichafu, kushika wanyama n.k. Kitendo cha kuosha mikono sio tu ni muhimu kwa watoto, bali hata kwa watu wazima. Uoshaji mikono ni muhimu kwa ajili ya kuzuia kupatwa na magonjwa mbalimbali, ambayo huweza kupatikana iwapo kanuni sahihi za usafi wa choo hazizingatiwi. Wakati mtoto anapofikia umri wa kwenda shuleni au kwenye shule ya chekechea, anatarajiwa kuwa na uwezo wa kutumia choo na kusafisha mikono yake mwenyewe baada ya kutoka msalani bila ya kusimamiwa na mtu.
Maambukizo ya fungus za miguuni na kichwani pia yanaweza kuzuilika iwapo uoshaji mikono sahihi utafuata. Watoto wanapaswa kuosha vizuri mikono yao, yani kati ya vidole na chini ya kucha, na ikiwezekana tumia brashi kusafisha mikono ya watoto. Ukaushaji vizuri wa mikono na vidole vile vile ni muhimu ili kuzuia maambukizo ya fungus. Watoto nao wanapaswa kuelewa umuhimu wa jambo hilo.
Usafi wa mwili unajumuisha pia usafi wa kucha. Wazazi wanapasa kuwakataza watoto tabia ya kutafuna kucha, kwani kucha za watoto mara nyingi huwa chafu na rahisi kubeba vijidudu maradhi. Kitendo cha kukata kucha za mtoto kitasaidi kupunguza kiwango cha vimelea vya maradhi vilivyoko chini ya kucha.
Tukiangalia usafi wa nywele tunaona kuwa, nywele za mtoto zinatakiwa kuwa fupi kama ni za kuchana na kama ni ndefu zinapaswa kusukwa mara kwa mara na kusafishwa vizuri kwa kutumia maji na sabuni au shampoo. Hii itasaidia kupunguza ringworm au chawa wa kichwani iwapo nywele zitakuwa chafu na kutooshwa vizuri. Watoto pia wanapaswa kushajiishwa kusafisha mikono yao kabla ya chakula, hii ni kwa sababu kitendo hicho kitasaidia kuzuia maambukizo ya magonjwa yanayoweza kuathiri mfumo wa chakula, wa kupumua na viungo vingine vya mwili. Nguo za mtoto pia ni lazima ziwe safi wakati wote , bila ya kusahau soksi, viatu na mahali anapolala. Mto anatakiwa kuvaa soksi kavu zisizo na unyevunyevu, ili kuzuia kuzaliana kwa fungus za miguuni. Avae viatu visivyobana, kama ni msimu wa joto mpatie viatu vilivyo wazi vyenye kupitisha hewa, mbadilishie mashuka yake anayolalia mara yakichafuka na kukifanya chumba au mahali anapolalia kuwa mahali safi na salama kwa afya yake. Mtengee mtoto taulo lake pekee yake, ili kuzuia maambukizo mbalimbali kama vile ya ngozi na kadhalika. Kwa kufanya hivyo ni matumaini yetu kuwa tutawaepusha watoto wetu na milipuko mbalimbali ya magonjwa.
Upangaji mzuri wa chumba cha kulala ni kuweka kitanda katikati. Wengi wetu tumezoea kukibana kitanda ukutani. Naamini ukiweka kitanda katikati (kama picha zinavyoonyesha) husaidia kurahisisha kufanya usafi wa chumba kwa kurahisisha kufagia uvunguni kila unaposafisha pia inafanya hewa izunguke vizuri na vilevile itakurahisishia kutandika.Kwa ujumla chumba chako kitapendeza.