Wednesday, 6 November 2013

SABABU ZINAZOZUIA KUOA/ KUOLEWA



SABABU INAYOWAFANYA WANAWAKE NA WANAUME WENGI KUTOTAKA
KUOA/ KUOLEWA.
Katika maisha ya vijana wengi wa sasa, tumekuwa kukishuhudia vitendo vingi vya ukatili kwa wanandoa kiasi ambacho tumepoteza imani sana katika kufikia maamuzi ya kuoa/ kuolewa.
Kwa muhtasari tuu, ningependa tuchambue sababu mbali mbali ambazo kiukweli zimekuwa kiongozi katika kuhakikisha thamani ya kuoa/ kuolewa inashuka au kupotea kabisa. Na kwa kila kijana ambaye anapenda kubadilika na kujifunza atapata kitu kipya katika makala hii na hivyo kufunguka kwa namna moja au nyingine katika swala hili gumu ambalo ndani ya miaka michache ijayo litakuwa janga la kitaifa.

Baadhi ya sababu hizo ni kama ifuatavyo;
-         Kuingia katika mahusiano ya kimapenzi kabla ya wakati, hii tukimaanisha katika umri mdogo.
-         Kushuhudia ukatili wa wazi wazi katika familia uliyoishi au jamii inayokuzunguka ndani na nje ya familia yako.
-         Kupata habari za kukatisha tamaa kutoka kwa wakubwa zako ambao kwa namna moja ama nyingine wamekuwa wakikushuhudia kushuka kwa thamani ya kuoa/ kuolewa.
-         Mfumo mbovu wa maisha unayoishi kijana, kwa kuamini kuwa vigezo na tabia unazohitaji kwa mke/ mume unayemtaka havijaonekana/ kukupendeza, hivyo unajikuta ukichagua sana.
-         Mara nyingine ni maudhi na kuumizwa nafsi kutoka kwa mpenzi aliekuacha/kumuacha bila sababu za msingi n.k
Kiukweli vijana wengi tuna mitazamo mbali mbali kulingana na uchaguzi sahihi juu ya nani anastahili/kufaa kuwa mwenzi wa maisha yangu, lakini tunakosea sana hasa inapokuja katika maamuzi,.

Nimeshuhudia vijana wengi wakipoteza muda katika kuchagua na kuandika vigezo vyao ambavyo wanahisi ndio key point ya kupata mwenzi, bila kusahau/ kuangalia upande mwingine wa shilingi, kwamba ‘ Mimi ninavigezo gani kulingana na hivi?’
Jiulize swali hili kijana unayesoma makala hii, wewe ni PERFECT? 

Na unahisi umekamilika sana kuwa na huyo unaemtaka? Mungu hawezi kukupa mwanamume/ mwanamke perfect kama wewe mwenyewe njia zako hazijatimilika.
Hivyo cha msingi hapa ni wewe kujitambua, kuangalia njia zako zipoje na sasa uingie katika swala la imani na kumuomba Mungu akupe mtu sahihi, ama sivyo utakuwa ukiwaona wanaume/wanawake wote ni wabaya/si waaminifu katika ndoa, na kubaki mpweke kwa maisha yako yote.
Jifunze kusamehe na kusahau, kisha fanya mambo yako kwa mpangilio utaona faaida zake.
Usife moyo tuzidi kuwa pamoja na tutafundishana na kusaidiana kila wakati,


Imeandaliwa na Diana D. Shirima
Founder - Wanawake Mashujaa Tanzania

No comments:

Post a Comment